1. UTANGULIZI |
| Mapambano dhidi ya rushwa si ya Serikali au Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na |
| Rushwa peke yake bali ni ya jamii nzima. TAKUKURU ina jukumu la kuongoza na |
| kushirikisha jamii nzima katika mapambano haya. TAKUKURU kupitia Idara ya Elimu |
| kwa Umma hutumia mbinu mbalimbali kuwaelimisha na kuwashirikisha wanajamii wa |
| makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na vijana walioko vyuoni katika mapambano dhidi |
| ya rushwa. |
| Vijana ni rasilimali ya taifa, watendaji wa sasa na siku zijazo na chachu ya mabadiliko |
| katika jamii. Umuhimu wa vijana ni wa kipekee katika kuleta mabadiliko ya kijamii |
| hususani katika kubadili mtazamo mzima wa rushwa kwa jamii ya kitanzania kutoka |
| kwenye mtazamo kuwa rushwa ni sehemu ya utamaduni na kuiona rushwa kuwa ni |
| tatizo la kitaifa lisilotakiwa kuvumiliwa kwa namna yoyote. Ili rasilimali hii iweze kutumika |
| vizuri zaidi, kuna umuhimu wa kuhamasisha uanzishwaji wa klabu hizi katika vyuo vya |
| elimu nchini. |
| TAKUKURU inatarajia kuzishirikisha klabu hizi katika mapambano dhidi ya rushwa kwa |
| namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha wanachama wa klabu hizi kwa njia |
| ya semina, matamasha ya sanaa, midahalo, kuwashirikisha wanachama wa klabu hizi |
| na walezi wao katika maadhimisho tunayoandaa na kushiriki na kuwashirikisha kwenye |
| vipindi vya redio na televisheni. |
| Aidha, ili kuwafikia na kuwaelimisha walengwa TAKUKURU itashirikiana na wadau |
| wengine wa mapambano dhidi ya rushwa ambao ni pamoja na Taasisi za dini, mashirika |
| ya umma, mashirika yasiyo ya kiserikali, asasi za kiraia na sekta binafsi. |
| 1 |
| 2. LENGO LA KUANZISHA KLABU |
| Klabu za wapinga rushwa katika vyuo zinaanzishwa kwa lengo la kuwajenga wanachuo |
| kimaadili na kuwashirikisha katika mapambano dhidi ya rushwa kwa :- |
| a) Kuwawezesha vijana kutambua nafasi na wajibu wao katika mapambano dhidi |
| ya rushwa na hivyo kushiriki ipasavyo katika kuzuia na kupambana na rushwa. |
| b) Kuwajenga vijana kimaadili kwa kuwafanya watambue madhara ya rushwa ili |
| waichukie katika maisha yao na kuchukua hatua za kuzuia na kupambana nayo |
| hatimaye kujenga jamii ya watu waadilifu. |
| c) Kuiwezesha jamii kutambua nafasi na wajibu wao katika mapambano dhidi ya |
| rushwa. |
| 3. UTAR ATIBU WA KUANZISHA KLABU |
| 1) Wanach uo wenye nia ya kuanzisha klabu wajikusanye na kuhamasisha |
| wanachuo wenzao umuhimu wa kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa. |
| 2) Wanachuo wachague wawakilishi watakaowasiliana na TAKUKURU kwa ajili ya |
| kupewa semina kuhusu rushwa na kuzindua klabu husika. |
| 3) Katika kila chuo kuwe na klabu moja tu hata kama idadi ya wanachama itakuwa |
| kubwa. |
| 4) Mkuu wa chuo ateue mwalimu mlezi wa klabu ambaye ni mwadilifu. |
| 5) Mwalimu mlezi aitishe kikao kwa ajili ya kuchagua viongozi wa klabu kwa njia ya |
| demokrasia. Viongozi hao ni mwenyekiti, makamu mwenyekiti na katibu. |
| 6) Shughuli zote zinazofanywa na klabu zisikiuke sheria, kanuni na taratibu za nchi |
| na zifahamike kwa uongozi wa chuo na TAKUKURU. |
| 7) Taarifa za utendaji wa klabu zitolewe kwa TAKUKURU kupitia kwa uongozi wa |
| chuo kisha kuwasilishwa Makao Makuu. |
| 8) Klabu iwe na katiba itakayoonyesha sifa za mwanachama, malengo, taratibu za |
| uchaguzi wa viongozi, idadi ya wanachama, ukomo wa uanachama. Aidha, |
| katiba iwasilishwe ofisi za TAKUKURU ili kuhakikiwa na baadae ithibitishwe na |
| kusainiwa na Mkuu wa Chuo. Katiba itawaongoza katika kutekeleza majukumu |
| ya klabu. |
| 2 |
| 4. SIFA ZA MWANACHAMA |
| 1. Awe mwanachuo wa chuo husika |
| 2. Awe mwadilifu |
| 3. Awe tayari kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa taarifa, |
| kutojihusisha na vitendo vya rushwa, kukemea vitendo vya rushwa na kuelimisha |
| wanafunzi wenzake na jamii kwa ujumla |
| 4. Atii sheria, kanuni na taratibu za chuo na nchi |
| 5. Awe na moyo wa kujituma, kujitolea na kushirikiana na wenzake. |
| 6. Ukomo wa uanachama kwa wanachama wa klabu za wapinga rushwa ni pale |
| mwanachuo anapohitimu masomo, anapojitoa mwenyewe au kutolewa kwa |
| sababu ya utovu wa nidhamu. |
| 7. Ukomo wa mwanafunzi kujiunga na klabu ni mwaka mmoja kabla ya kuhitimu |
| masomo. |
| 5. SIFA ZA KIONGOZI |
| 1. Awe mwanachama wa klabu kwa muda usiopungua miezi 6. |
| 2. Awe anashiriki katika shughuli zote za klabu. |
| 3. Awe na uwezo wa kujieleza, ujasiri, uwazi na ukweli. |
| 4. Awe mwepesi wa kusikiliza na kutoa maamuzi katika masuala yote ya klabu. |
| 5. Uchaguzi ufanyike mara moja kila mwaka. |
| 6. Nafasi za uongozi ziwe 3 tu ( mwenyekiti, makamu mwenyekiti na katibu). |
| 7. Asiwe mwanachama aliye katika mwaka wa mwisho wa masomo. |
| 6. MIKUTANO |
| 1. |
| Mikutano ya kujadili maendeleo na masuala mbalimbali ya klabu ifanyike |
| kulingana na utaratibu mtakaojiwekea kwa kufuata ratiba za masomo. |
| 2. |
| Iwapo kuna dharura viongozi wa klabu wanaweza kuitisha kikao cha dharura kwa |
| kutoa taarifa ya muda mfupi kwa wanachama. |
| 7. SHUGHULI ZA KUFANYA |
| 1) Kujielimisha na kujua haki za raia. |
| 3 |
| 2) Kuelimisha wanachuo wenzao na jamii kwa ujumla kuhusu maana ya rushwa, |
| sababu za kuwepo kwa rushwa, madhara ya rushwa na umuhimu wa kuzuia na |
| kupambana na rushwa. |
| 3) Kufanya midahalo ndani na nje ya chuo kuhusu rushwa. |
| 4) Kufanya mijadala ya wazi itakayoibua hoja na changamoto mbalimbali kuhusu |
| mapambano dhidi ya rushwa. |
| 5) Kufanya maonyesho ya sanaa yenye ujumbe wa mapambano dhidi ya rushwa |
| kwa njia ya nyimbo, maigizo, ngonjera na nyinginezo. |
| 6) Kushiriki katika shughuli za kijamii. |
| 7) Kushiriki kuandika insha, makala, kuchora katuni na hadithi mbalimbali zenye |
| maudhui ya kuelimisha na kukemea rushwa. |
| 8) Kutoa taarifa za vitendo vya rushwa TAKUKURU. |
| 9) Kushiriki katika maonesho, matamasha na makongamano mbalimbali |
| yatakayoandaliwa na TAKUKURU au Asasi nyingine kwa ajili ya kueneza ujumbe |
| wa kushirikisha jamii kupambana na rushwa. |
| 10) Kujifunza utendaji kazi katika sekta ya umma na binafsi kwa kuwaalika viongozi |
| wa sekta kuongea nao wakati wa vikao vyao kwa lengo la kupanua uelewa wa |
| haki na wajibu wao katika huduma mbalimbali zitolewazo kwa wananchi. |
| 11) Kushirikiana na Kamati za Uadilifu zilizoanzishwa katika halmashauri zenu kwa |
| kutoa taarifa za ukiukwaji wa maadili. |
| 12) Kushirikiana na Kamati za Uadilifu zilizoanzishwa vyuoni kujenga maadili katika |
| vyuo. |
| 8. HITIMISHO |
| Ni wazi kuwa vijana ni hazina muhimu ya taifa. Umuhimu wao katika jamii yoyote ni |
| chachu pekee ya kuleta mabadiliko ya kijamii, kisiasa, kiuchumi na kimaendeleo, ili |
| kujenga kizazi kisichovumilia wala kukumbatia rushwa katika kutekeleza majukumu |
| yake. |
| Mafanikio ya mapambano dhidi ya rushwa yanategemea kijana kwani kukataa |
| kwako rushwa kuna thamani. Aidha, uadilifu wako na wangu utaitokomeza rushwa. |
| 4 |
No comments:
Post a Comment